Thursday, May 28, 2009

Freeman Mbowe Fisadi Papa


JE NI KWELI MBOWE NI FISADI PAPA?



Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe ni mmoja kati ya mafisadi wazoefu hapa nchini. Alianza ufisadi huo miaka mingi iliyopita tangu alipokuwa karani wa mahesabu katika Benki Kuu akiwa chini ya baba mkwe wake, Edwin Mtei aliyekuwa Waziri wa Fedha, wakati huo, kabla hajatimuliwa na Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, mwaka 1979 kwa kulazimishwa ajiuzulu.

Kati ya mwaka 1993 na 1994, Mbowe alizama zaidi katika ufisadi akisaidiana na dada yake, Selina, aliyekuwa akifanya kazi Telex Room katika Benki Kuu kwa kushirikiana naye kutorosha fedha za kigeni kwenda nje ya nchi wakitumia akaunti ya Mhindi mmoja anayeitwa Shiraz aliyekuwa na akaunti yake huko London, Uingereza.

Selina ambaye baada ya kuiba sana na kaka yake na kukaribia kunaswa alikimbilia Marekani ambako amekuwa akiishi kwa miaka mingi iliyopita anahofia kurudi kutokana na dhambi aliyoitendea Tanzania.

Takwimu za ufisadi wa Mbowe zimejaa uharamia mkubwa kwa taifa, hivyo haieleweki kuona hivi leo anatumia kivuli cha Chadema kufichia uovu wake kwa Watanzania alioshiriki kwa miaka mingi kuwaibia fedha zao na kutaka aonekane kuwa ni kiongozi mwadilifu na pia mwenye uchungu mkubwa na raslimali za nchi yetu.

Kama Mbowe anabisha kuhusu ufisadi wake huo natoa changamoto kwake awaeleze wananchi undani na ukweli wa alivyokopa shilingi milioni 800 katika Benki ya Greenland, akachangia kuifilisi kinyume na maelezo aliyotoa hivi karibuni kwa waandishi wa habari akidai eti kuwa deni hilo alilipa huku akijua kwamba ni muongo.

Watu wanaelewa alivyofanya hila na mbinu chafu kuhakikisha documents zilizokuwa na kumbukumbu za mkopo wake zinaibwa kutoka benki hiyo na kupelekewa, akazichoma moto ili kupoteza kabisa ushahidi, jambo alilofanikiwa na ndiyo maana leo anaweza kusema kwa kujiamini kwamba alikopa na kulipa deni zima.

Kuiba nyaraka za mkopo na kuzichoma moto ili zisiwepo kabisa ndiko kulipa deni hilo?!

5 comments:

YoYo said...

wewe hachana na mbowe. kuma la mama yako we msenge, CCM inakwisha hata mkileta ufisadi wenu kwenye globu yetu

Anonymous said...

Huyu NAYE NI MWIZI INABIDI AENDE SEGEREA MCHAGA JAMBAZI

Anonymous said...

Jamani mie kwa mtazamo mpaka saivi bado sioni kuna mtu ambaye si fisadi.Watu wengi wamekuwa wakipinga usifasi wakati wakiwa nje ya system lakini mara tu baada ya kuingi katika system basi wao ndio wanakuwa mafisadi number moja.
Hali hii hata katika jamii yetu imezoeleka.Yaani kama mtu akiwa madilifu na kufanya kazi bila kuiba,mara tu baada ya kustafu kama atakuwa hana kitu basi utasikia watu wakimsema eti jamaa mjinga sana yule alikuwa waziri kwa mda wa miaka kumi lakini hakuna alichokifanya.

Anonymous said...

We uliyeandika hii post umeshindwa kuondoa harufu za "POROJO" kwenye habari yako. Inaonekana kama ulikaa chumbani na kutunga insha.
Shenzi we...kafie mbali na CCM yako.

Anonymous said...

Kweli blog hii inatowa maoni kwa wote!!! du hata mbowe? ingekuwa ile blog ya nanihii halafu uwkandie ccm! inatupwa kapuni. powa jino kwa jino tu jamii forum